Teuvo Kopra
www.teuvokopra.fi
Suomi            Tanzania

Teuvo Kopra:


Maana ya majina ya Biblia



A

Abramu = Baba aliyeinuliwa

Adamu = Mwanadamu. Wanadamu. Mwekundu

Agabo = Kupenda

Agagi = Mwenye fitina

Agripa = Farasi mwitu

Ahabu = Ndugu ya baba

Ahasuero = Mtawala. Mfalme

Ai = Maporomoko

Akani = Ajali. Msababishji wa ajali

Akila = Tai

Amori = Wa-mlima

Amosi = Aliyesumbuliwa. Mbeba mzigo. Mwenye nguvu.

Anania = Yehova ni mwenye neema

Anasi = Mungu ni wahuruma

Andrea = Mwanamume

Apolo = Miungu wa Waapolonia

Areopago = Vilima vya (mungu) Aresi

Arkipo = Mtawala wa farasi

Asa = Daktari. Mponyaji

Asafu = Mkusanyaji

Asheri = Heri. Mwenye heri

Athene = Mji wa (mungu) Athene

Augusto = Anayestahili sifa

Ayubu = Anayechukiwa. Mwenyekutubu


B

Babeli = Anayeingiza kwenye vurugu. Mvurugaji

Balaamu = Mgeni

Balaki = Mwangamizaji

Barnaba = Kijana wa faraja

Bartholomayo = Mwana wa Talmai

Bartimayo = Mwana wa Timayo

Bath-sheba = Binti wa kiapo. Binti wa saba

Beelzebuli = Bwana wa inzi

Beer-sheba = Kisima ya kiapo. Kisima ya saba

Belshaza = Mfalme alindwa (mungu) Beel

Belteshaza = Beel (mungu) alinda uhai wake

Benyamini = Mwana wa furaha (yaani mwana wa mkono wa kulia)

Bethania = Kijiji cha maskini

Betheli = Nyumba ya Mungu

Bethfage = Sehemu ya kutunza mizabibu mabichi

Bethsaida = Eneo la kuvua samaki

Bethzatha = Nyumba ya upole

Betlehemu = Nyumba ya mikate

Boanerge = Wana wa ngurumo

Bonde la Akori = Ajali


D

Dani = Hakimu

Danieli = Mungu ni hakimu wangu

Dario = Mtawala. Anayechipusha

Daudi = Anayependwa

Debora = Nyuki

Dekapoli = Mji wa kumi

Delila = Anayependa kujipendekeza

Dema = Mwanaume wa watu


E

Eben-ezeri = Jiwe la msaada

Edeni = Uzuri

Edomu = Nyekundu

Efeso = Anayetamaniwa. Anayetakwa

Efraimu = Tunda lenye sehemu mbili. Mwenye matunda

Eli = Mungu wangu

Elimeleki = Mungu ni mfalme

Elimu = Miti ya mitende. Mikaratusi

Elisabeti = Mungu wa kiapo. Mungu ni kiapo

Elisha = Mungu ni wokovu

Eliya = Yehova ni Mungu

Emau = Vizima moto

Epafra = Kwa mungu jike wa Afrodite

Erasto = Anayependwa

Esau = Mwenye nywele

Esta = Nyota. Mungu wa kike

Ezekieli = Mungu ni mwenye nguvu. Mungu anatia nguvu

Ezra = Msaada


F

Farao = Nyumba kubwa

Feliki = Mwenye furaha

Festo = Mwenye sherehe

Filadelfia = Upendo wa ndugu

Filemoni = Mwenye upendo. Mkarimu

Filipo = Rafiki wa farasi. Anayependa farasi

Filisti = Kutoka

Foinike = Nchi ya mitende


G

Gabrieli = Mtu wa Mungu

Gadi = Furaha. Bahati

Galilaya = Eneo. Sehemu

Gamalieli = Zawadi ya Mungu. Mungu anatoa thawabu

Gathi = Kinu ya kukamulia zabibu

Gaza = Nguvu. Ushujaa

Gehazi = Bonde la maono

Genesareti = Bustani za watawala

Gershoni = Aliyefukuzwa. Mgeni

Gethsemane = Chombo cha kukamulia mafuta

Gideoni = Anayepiga hadi kufa.

Gileadi = Nguvu. Ngumu

Gilgali = Duara

Golgotha = Fuvu

Gomora = Gharika


H

Habakuki = Kumbatia

Habili = Uvumi wa upepo. Mbuga

Hagai = Penye sherehe

Hajiri = Kimbia. Uhamaji. Safari

Hamu = Moto. Vuguvugu. Giza. Nyeusi

Hana = Aliyerehemiwa

Har-Magedoni = Mlima wa Har-Magedoni

Harani = Njia. Mtaa

Haruni = Aliyeangaza. Anayeangaa

Hawa = Uhai

Hebroni = Umoja

Henoko = Aliyeolewa. Kuweka wakfu

Hermoni = Patakatifu

Herode = Shujaa. Mungu nusu

Herodia = Shujaa

Hezekia = Mungu ni nguvu yangu

Hidekeli = Tigris = Mkali na anayekwenda kasi. Panapootesha mtende

Horebu = Pakavu. Pasipo na kitu

Hosana = Wokovu. Atoaye afya. Anayetoa maendeleo.

Hosea = Wokovu

Huri = Shimo. Mweupe. Amezaliwa kwa uhuru.


I

Ibrahimu = Baba wa wengi

Imanueli = Mungu pamoja nasi

Isakari = Yeye anatoa ajira. Ananipa mshahara

Isaya = Yahwe anaokoa. Yahwe ni wokovu

Ishmaeli = Mungu anasikia maombi

Iskariote = Mwanamume wa Kerioti. Mtumia kisu

Israeli = Mungu anapigana. Anapigana na Mungu


K

Kadeshi = Patakatifu. Palipowekwa wakfu

Kaini = Aliyepatikana. Mkuki.

Kaisaria = Wa kaisari

Kalebu = Mbwa

Kana = Bomba la tawi

Kapernaumu = Kijiji cha Nahumu

Karmeli = Bustani (ya Mungu)

Kayafa = Bonde dogo. Anayetafsiri ishara

Kefa = Mwamba

Kenkrea = Mji wa mtama

Kerithi = Iliyokatwa

Kishi = Upinde

Kishoni = Iliyojipinda. Iliyo na mapindo

Kolosai = Mji wa sanamu

Kornelio = Mwenye pembe

Krispo = Nywele zenye mawimbi


L

Labani = Mweupe

Laodikia = Utawala wa watu

Lawi = Umoja. Nia moja

Lazaro = Eleasar = Mungu ni msaada. Mungu amesaidia

Lea = Aliyechoka. Mwenye nguvu. Malkia wa nyumba

Lebanoni = Mweupe

Luka = Mwanga. Kuangaza

Lutu = Shera. Pazia


M

Magdalene = Anayetoka Magdala

Malaki = Malaika wangu. Mpeleka ujumbe

Mamra = Mafuta. Unene

Manase = Yeye (Mungu) amenifanya kusahau

Mariamu = Uchungu. Ubishi

Martha = Malkia

Mathayo = Zawadi ya Yehova

Melkizedeki = Mfalme wa busara

Methusela = Mtu wa mkuki

Midiani = Hukumu. Mapambano

Mika, Mikaya = Nani kama Yehova

Mikaeli = Nani anayelingana na Yehova

Miriamu = Uchungu. Ubishi

Mlima wa Mizeituni = Kinu cha kukamulia zabibu

Moabu = Kutoka kwa baba (baba wa mama)

Moleki = Mfalme

Mordekai = (Miungu) kwa Marduki. Kutoka Marduki

Moria = Mungu anajitokeza. Aliyeonwa na Mungu

Musa = Anayevutwa juu


N

Naamani = Uzuri. Anayependeza

Nadabu = Anayejitoa. Mzuri

Naftali = Mapambano. Vita vyangu

Nahumu = Anayeleta faraja

Naini = Mzuri. Kupendeza

Naomi = Uzuri wangu. Anayenipendeza. Mzuri

Nathanaeli = Mungu ametoa

Nathani = Yeye (Mungu) ametoa

Nazareti = Mwenye matawi mengi. Mtawala wakike

Nebukadneza = Nabu (mungu) anayelinda mipaka

Nehemia = Yehova anafariji

Nikodemo = Mshindi wa mtaifa

Nile = Mto. Gharika. Mkondo

Nuhu = Mapumziko


O

Obadia = Mtumishi wa Yehova

Onesimo = Mwenye faida. Anayesababisha baraka


P

Paulo = Mdogo

Penina = Ushanga

Penueli = Uso wa Mungu

Pergamo = Maisha ya ndoa

Petro = Jiwe. Mwamba

Pilato = Aliyejiandaa kwa mkuki

Potifa = Mkuu wa walinzi

Potifera = Zawadi ya Ra (mungu wa jua)

Prisila = Priska mdogo

Priska = Mzee. Anayestahili heshima

Publio = Wa-watu


R

Rabi = Bwana wangu

Raboni = Bwana wangu (mkuu kuzidi Rabi)

Rahabu = Paana

Raheli = Kondoo jike

Rebeka = Mtego. Anayejipendekeza

Reubeni = Yeye (Bwana) ameona unyonge wangu. Angalieni kijana

Rumi = Mji wa vilima saba

Ruthu = Urafiki


S

Safira = Mzuri. Anayependeza

Salemu = Mpole. Tengamaa

Samaria = Ulinzi. Eneo la ulinzi

Samsoni = Mwenye nguvu. Mwenye mwanga

Samweli = Aliyesikilizwa na Mungu.

Sanbalati = Sin (mungu) amemfanya awe na uhai

Sara = Anayetawala. Malkia

Sarai = Ukoo wa kifalme

Sarepta = Mahali pa usafisho

Sauli = Aliyeombwa

Sayuni = Ngome. Maangamizi. Mahame

Sefania = Yehova anaficha. Yehova ameficha

Sefari = Anaunguza. Juu. Aliyeinuliwa

Senakeribu = Sin (mungu) ameongeza hesabu za wandugu

Sethi = Aliyewekwa sehemu ya pili. Kulipizwa

Sharoni = Tambarare

Shekemu = Mabega. Mgongo

Shemu = Jina

Shushani = Ua

Sidoni = Aliyezungukwa na ngome. Kuvua samaki

Sikari = Mlevi

Sila = Amepatwa kwa maombi

Siloamu = Aliyetumwa

Silwano = Mungu wa msituni

Simeoni = Kusikiliza maombi

Simoni = Kusikiliza maombi

Sinai = Kichaka chenye miiba

Sintike = Mwenye furaha. Msaidizi

Sipora = Ndege (mdogo)

Sirti = Mchanga

Skewa = Kushoto

Smirna = Manemane. Mateso

Sodoma = Iliyounguzwa (chomwa). Sehemu yenye chokaa

Stefana = Aliyevikwa taji.

Stefano = Taji

Sulemani = Mpole


T

Tabitha = Swala

Tabori = Mlima

Tarshishi = Jiwe la thamani. Lulu

Tera = Swala wa mlimani

Tertio = Wa-tatu

Tertulo = Wa-tatu

Theofilo = Rafiki ya Mungu

Tikiko = Mwenye furaha

Timayo = Aliyeheshimiwa. Mwenye heshima

Timotheo = Anayeheshimu Mungu

Tiro = Mwamba

Tobia = Yehova ni mzuri

Tomaso = Pacha

Trofimo = Anayekuzwa


U

Urimu na Thumimu = Ukamiliki na nuru

Uru = Nuru. Miali (ya moto)

Uyahudi = Nchi ya Mwayahudi


W V

Waebrania = Wanatoka pande zingine. Wavuka mpaka. Wageni

Wafilisti = Wanaotoka

Vashti = (Mwanamke) mzuri


Y

Yafethi = Yeye anapanua

Yairo = Yeye anaangaza

Yakobo = Anayeshika kisigino. Msaliti

Yeftha = Yeye (Mungu) anafungua

Yeremia = Mungu ni mkuu. Mungu anainua.

Yeriko = Mji wa manukato. Mji wa mwezi mpya

Yeroboamu = Mataifa watakuwa wengi. Taifa litapigana.

Yerusalemu = Msingi wa amani. Nyumba ya amani.

Yesu = Yoshua = Mungu anaokoa. Mungu ni wokovu

Yezebeli = Ambaye hajaolewa. Kuinua

Yezreeli = Mungu anapanda

Yoabu = Yehowa ni baba

Yoashi = Bwana anatoa. Bwana anakuja (kusaidia)

Yoeli = Bwana ni Mungu

Yohana = Yehova ni wa huruma

Yona = Njiwa

Yonathani = Yehova ametoa

Yordani = Unawaanguka. Unawatelemka

Yoshua = Yesu = Yehova anaokoa. Yehova ni wokovu

Yuda = Yeye (Bwana) ashukuriwe. Anayeshukuriwa

Yusufu = (Bwana) anaongeza. Anafukuza


Z

Zabuloni = Makao. Pakuishi. Nyumbani

Zakaria = Yehova amekumbuka

Zebedayo = Zawadi ya Mungu. Mungu ni zawadi

Zekaria = Yehova amekumbuka

Zena = Zawadi ya Zeus (miungu)






Copyright Teuvo Kopra




WebDesign Miia Metsola