Teuvo Kopra
www.teuvokopra.fi
Suomi            Tanzania

Teuvo Kopra:

Kronologia ya Biblia

Miaka ya matukio mbali mbali katika Biblia.

 

Dibaji.

 

Kronologia ni mtiririko wa mambo yaliyotokea zamani, katika historia. Kwa sababu Biblia hajaandikwa katika mpangilio wa kikronologia, vivyo hivyo uhakika kamili haupo katika mipangilio ya matukio haya kwa usahihi kamili. Mfano tukiangulia wakati wa wafalme ni vigumu kupata uhakika wa utawala sababu wakati mwingi wafalme walitawala hata wawili au watatu, baba na mwana. Kijana aliweza kutawala ingawa baba alikuwepo bado anaishi.


Wataalamu wa historia wamechunguza wakati wa Biblia. Wamefaulu kupata na kuelewa mambo mengine yanayotusaidia katika kujua kuhusu matukio mbali mbali katika Biblia, lakini mambo mengine bado, hayajachunguzwa. Katika Biblia kuna vipengele vingine vinavyoweza kupata mwelekezo juu ya matukio. Wataalamu wa historia wameichunguza Biblia na historia na wanaelewa kwamba Sulemani alitawala miaka ya 972-932 kabla ya Kristo. (K.K.) Utawala wake uliendelea kwa miaka 40. (1Fal 11:42) Ufalme wa Israeli uligawanyika mara baada ya utawala wa Sulemani, kama mwaka wa 932 K.K.


Sulemani alianza kujenga Hekalu katika mwaka wa nne wa utawala wake, yaani mwaka wa 969/968 K.K. Kujenga kulianza mwaka wa 480 baada ya wana wa Israeli kuliondoka Misri. (1Fal 6:1) Wana wa Israeli waliondoka Misri mwaka wa 1448 K.K. (968 + 480 = 1448) Waisraeli walikaa Misri miaka 430. (Kut 12:40) Wakati huo mateso yalichukua miaka 400. (MDO 7:6) Waliingia Misri mwaka wa 1878 K.K. (1448 + 430 = 1878) Kuingi Misri ni wakati ule Yakobo alipoingia na familia yake. Wakati huo Yusufu alikuwa amepandishwa cheo katika nyumba ya Farao. Baadaye alipoteza kazi yake ya utawala kwa sababu Misri ilipata Farao mwingine. Baadaye mateso yalianza na Waisraeli walikuwa watumwa katika nchi ya Misri.


GAL 3:16,17 inatueleza kuhusu ahadi iliyopewa Ibrahimu, (MWA 22:18) na pia Yakobo alivyohakikishiwa kuhusu ahadi hiyo. (MWA 46:2-4) Yakobo alihakikishiwa ahadi hiyo alipoingia Misri, katika mwaka wa 1878. Baada ya miaka 430 Yakobo alipoingia Misri, sheria ilitolewa kwa Waisraeli. Ilitolewa 1448/1447. Wakati huo wana wa Israeli walikuwa wameanza safari yao kuelekea nchi ya ahadi. Wakati wa Waamuzi wana wa Israeli walikuwa wamekaa katika nchi yao miaka 300. (AMU 11:26)


Hapa tunakwenda kuona jinsi mambo yalivyoendelea.

Pia tutaona historia kidogo ingawa hatuna uhakika na mipangilio ya miaka. Inatubidi kuchunguza kwa makini kuhusu mambo haya: "Hajui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua." (1KOR 8:2) "Tunafahamu kwa sehemu". (1KOR 13:9) Hivyo inatubidi kufanya uchunguzi kwa makini sana.

 

Mipangilio ya miaka katika Biblia baada ya kuumbwa kwa Adamu

 

(B.A. = Baada ya Adamu)

(K.K. = Kabla ya Kristo)

 

 

MWANZO.

Tangu mwanzo hadi 1807 K.K. (Kabla ya Kristo)

 

000

Kuumbwa kwa Adamu. Aliishi miaka 930. Alifariki mwaka 930 baada ya kuumbwa kwake. (MWA 1:27-5:5)

Kaini na Habili walizaliwa. Baadaye Kaini alimwua Habili. Inawezekana watoto wengine pia walikuwa wamezaliwa.

Kabla ya gharika watu wote na wanyama walikula majani ya miche (MWA 1:29,30). Baadaye walikula pia nyama. (MWA 9:3)

 

130 B.A.

Sethi alizaliwa. Aliishi miaka 912. Alifariki mwaka wa 1042. B.A. (MWA 5:3-8)

 

235 B.A.

Enoshi alizaliwa. Aliishi miaka 905. Alifariki mwaka wa 1140. B.A. (MWA 5:6-11) Hapo ndipo watu walianza kuliitia jina la Bwana. (MWA 4:26)

 

325 B.A.

Kenani alizaliwa. Aliishi miaka 910. Alifariki mwaka wa 1235. B.A. (MWA 5:9-14)

 

395 B.A.

Mahalaleli alizaliwa. Aliishi miaka 895. Alikufa 1290. B.A. (MWA 5:12-17)

 

460 B.A.

Yaredi alizaliwa. Aliishi miaka 962. Alikufa mwaka wa 1422 B.A. (MWA 5:15-20)

 

622 B.A.

Henoko alizaliwa. Aliishi miaka 365. Alipotembea pamoja na Mungu miaka 300, hakuwepo tena kwani Mungu alimchukua katika mwaka wa 987 B.A. (MWA 5:18-24)

 

687 B.A.

Methusela alizaliwa. Aliishi miaka 969. Aliishi miaka mingi zaidi duniani. Alikufa mwaka ule wa gharika 1656 B.A. (MWA 5:21-27)

 

874 B.A.

Lameki alizaliwa. Aliishi miaka 777. Alifariki mwaka 1651 B.A. (MWA 5:25-31)

 

930 B.A.

Adamu alifariki. Akiwa na miaka 930. (MWA 5:5)

 

987 B.A.

Henoko alichukuliwa na Mungu. Akiwa na miaka 365. (MWA 5:22-24)

 

1042 B.A.

Sethi alifariki akiwa na miaka 912. (MWA 5:8)

 

1056 B.A.

Nuhu alizaliwa. Aliishi miaka 950. Alifariki mwaka wa 2006 B.A. (MWA 5:28-9:29)

 

1235 B.A. Kenani alifariki akiwa na miaka 910. (MWA 5:14)

 

1290 B.A.

Mahalaleli alifariki akiwa na miaka 895. (MWA 5:17)

 

1422 B.A.

Yaredi alifariki akiwa na miaka 962. (MWA 5:20)

 

1558 B.A.

Shemu alizaliwa. Aliishi miaka 600. Alifariki mwaka wa 2158 B.A. (MWA 5:32-11:11)

 

1651 B.A.

Lameki alifariki akiwa na miaka 777. (MWA 5:31)

 

1656 B.A.

Gharika. Ilichukua mwaka mmoja na siku kumi. (MWA 6:7-8:19) Matokeo ya gharika yameonekana huko Tigri (= Hidekeli) na mkondo wa mto Frati.

 

1658 B.A.

Arfaksadi alizaliwa. Aliishi miaka 438. Alikufa 2096 B.A. (MWA 10:22, 11:10-13)

 

1693 B.A.

Sela alizaliwa. Aliishi miaka 433. Alikufa 2126 B.A. (MWA 10:24, 11:12-15)

 

1723 B.A.

Eberi alizaliwa. Aliishi miaka 464. Alikufa mwaka wa 2187 B.A. (MWA 11:14-17)

 

1757 B.A.

Pelegi alizaliwa. Aliishi miaka 239. Alikufa 1996 B.A. (MWA 11:16-19) Wakati wa Pelegi dunia iligawanyika (MWA 10:25)

 

1787 B.A.

Reu alizaliwa. Aliishi miaka 239. Alikufa 2026 B.A. (MWA 11:18-21)

 

1819 B.A.

Serugi alizaliwa. Aliishi miaka 230. Alikufa 2049 B.A. (MWA 11:20-23)

 

1849 B.A.

Nahori babu ya Abramu (=Ibrahimu) alizaliwa. Aliishi miaka 148, alifariki 1997 B.A. (MWA 11:22-25)

 

1878 B.A.

Tera baba ya Abramu (=Ibrahimu) alizaliwa. Aliishi miaka 205. Alifariki 2083 B.A. (MWA 11:24-32)

 

1948 B.A.

Abramu alizaliwa. Aliishi miaka 175. Alifariki 2123 B.A. = 1993 K.K (MWA 11:26-25:8)

 

 

Tangu hapo miaka kabla ya Kristo: (K.K.)

 

2168 K.K. (Kabla ya Kristo)

Abramu alizaliwa Uru wa Wakaldayo. (MWA 11:26) Tera, baba yake alikuwa na miaka 70.

Wakati wa Abramu Nuhu aliishi miaka 58, na Shemu miaka 210. (Shemu alifariki miaka 35 baada ja kifo cha Ibrahimu = Abramu).


Inawezekana kwamba Shemu ndiye Melkizedeki. (MWA 14:18-20)

Baada ya kuzaliwa kwa Abramu, Arfaksadi aliishi miaka 148, Sela aliishi miaka 178, na Eberi miaka 239, na Pelegi miaka 48, na Reu 78, na Serugi miaka 101, na Nahori miaka 49, na Tera 135, baada ya kuzaliwa kwa Abramu. Hivyo vizazi vilivyoishi ni 11 kwa wakati mmoja.

 

2158 K.K.

Sarai alizaliwa. Sarai pia alikuwa binti wa Tera (MWA 20:12). Abramu alimzidi Sara miaka kumi. (MWA 17:17)

 

2118 K.K.

Tera, Abramu na Lutu waliondoka kutoka nchi ya Uru wa Wakaldayo mpaka Harani. (MWA 11:31)

 

2110 K.K.

Nuhu alifariki akiwa na miaka 950.

 

2093 K.K.

Abramu na Lutu walitoka Harani baada ya kukaa huko miaka 24. (MWA 12)

Tera alibaki huko na alikufa baada ya miaka 60 huko. (MWA 12:1-5)

 

2092 K.K.

Abramu aliondoka kwenda Misri akae huko kwa kipindi cha njaa. (MWA 12:10-13:1)

 

2090 K.K.

Abramu na Lutu walitengana. (MWA 13:5-12)

 

2085 K.K.

Vita katika Bonde la Sidimu. Lutu pamoja na jamaa yake walichukuliwa mateka. Abramu alipigana na ndiye aliyeshinda vita na Abramu alishinda, na akamrudisha Lutu. Baadaye Abramu alikutana na Melkisedeki (Shemu?) (MWA 14)

 

2084 K.K.

Bwana alimtokea Abramu. (MWA 15)

 

2082 K.K.

Ishmaeli alizaliwa. (MWA 16)

 

2069 K.K.

Abramu alipewa jina Ibrahimu na Sarai akaitwa Sara. (MWA 17:5,15)

Tohara. (MWA 17:10,23-27)

Mungu aliangamiza Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu kwa moto na kiberiti. (MWA 19, KUM 29:23)

 

2068 K.K.

Isaka alizaliwa. (MWA 22:1-3) Ibrahimu alikuwa na miaka 100 na Sara miaka 90 Isaka alipozaliwa. (MWA 21:5, 17:17)

 

2050 K.K.

Ibrahimu alimtoa Isaka dhabihu. (MWA 22:1-19)

 

2033 K.K.

Tera baba yao Ibrahimu na Saara alifariki. (MWA 11:32)

 

2031 K.K.

Sara alifariki huko Hebroni akiwa na miaka 127, miaka miwili baada ya kifo cha baba yake. (MWA 23:1,2)

 

2028 K.K.

Isaka alimwoa binti wa Bethueli Rebeka. (MWA 22:20-23, MWA 24)

 

2008 K.K.

Mapacha Esau na Yakobo walizaliwa. (MWA 25:20-26)

 

1993 K.K.

Ibrahimu alifariki. (MWA 25:8) Esau na Yakobo walikuwa na miaka 15.

 

1968 K.K.

Esau alioa binti wa Wahiti Yudithi na Basemathi akiwa na miaka 40. (MWA 26:34)

 

1958 K.K.

Shemu (Melkisedeki?) mwana wa Nuhu alifariki akiwa na miaka 600. Ilitokea miaka 35 baada ya kifo cha Ibrahimu.

 

1945 K.K.

Ishmaeli alikuwa na miaka 137 wakati wa kifo chake. (MWA 25:17)

 

1931 K.K.

Yakobo alikwenda kwa Labani, mjomba wake, akiwa na miaka 77. (MWA 28:10-29:13)

 

1924 K.K.

Yakobo aliwaoa binamu zake Lea na Raheli akiwa na miaka 84. (MWA 29:17-28)

 

1917 K.K.

Yusufu alizaliwa. (MWA 30:22-24)

 

1911 K.K.

Yakobo na jamaa yake walitoka kwa Labani kurudi nchi ya Kanani. (MWA 31-35) Inawezekana mama yake alikuwa amekwisha kufariki na baba yake Isaka alikuwa na miaka 157.

 

1905 K.K.

Benyamini alizaliwa.

Raheli alifariki. (MWA 35:17-19)

 

1900 K.K.

Yusufu aliingia Misri akiwa kama mtumwa kwa Potifa akiwa na miaka 17. (MWA 37: 28,36)

Potifa alikuwa farao Sesostris II (1903-1887) mfanyakazi wa ndani na mkuu wa aliyeangalia usalama.

 

1891 K.K.

Yusufu alifungwa. (MWA 39:20)

 

1888 K.K.

Isaka alifariki akiwa na miaka 180. (MWA 35:28,29)

 

1887 K.K.

Yusufu alipelekwa mbele ya farao Sesostris III (Farao alitawala 1887-1849) (MWA 41:14)

 

1887-1880 K.K.

Ilikuwa miaka ya mavuno (MWA 41:47)

 

1880-1873 K.K.

Ilikuwa miaka ya njaa. (MWA 41:54)

 

1879 K.K.

Ndugu zake Yusufu walikwenda Misri mara ya kwanza. (MWA 42)

 

1878 K.K.

Yakobo alikwenda Misri. Alikutana na Yusufu baada ya kutengana miaka 22. Yakobo aliishi miaka 17 baadaye. (MWA 46)

 

1861 K.K.

Yakobo alifariki akiwa na miaka 147. (MWA 47:28, 49:33)

 

1849 K.K.

Yusufu alipoteza kazi na mamlaka yake kwa sababu farao Sesostris III alifariki na farao Amenemhet III alianza kutawala.

Hapo wana wa Israeli walianza kuteswa na mateso yalichukua miaka 400. (MDO 7:6)

Nayo yaliendelea mpaka mwaka wa 1448 K.K., wakati huo wana wa Israeli walitoka Misri.

 

1807 K.K.

Yusufu alifariki akiwa na miaka 110. (MWA 50:26)

Mwisho wa kitabu cha MWANZO.

 

Tangu mwaka wa 1807 K.K. hadi mwaka wa 1558 K.K. ilikuwa katikati ya MWANZO na KUTOKA na ilikuwa miaka 250. Biblia haisemi mambo yaliyotokeo hapo katikati. Wakati huo wana wa Israeli waliongezeka huko Misri. Waliishi kwenye jimbo la Gosheni.

Jamii ya kifalme Babeli wa kwanza ilitawala. (1894-1595) Hammurabi, mwanasheria maarufu, alikuwa mfalme (1792-1750 K.K.).


Kwenye mwaka wa 1730 kabila la Hyksos liliwatawala Wamisri. Lilikuwa na magari ya farasi ya kivita na hivyo Wamisri hawakuweza kitu. Kabila la Hyksos lilitawala Misri miaka 150. Kabila la Hyksos lilitoka kaskazini na lilikuwa jamaa ya Shemu. Huko Misri, katika mji wa Thebe farao Sekenenre (1600 K.K.) alipigana na kabila la Hyksos lakini aliuawa katika mapigano. Inawezekana aliuawa wakati wa vita. Fuvu la kichwa chake kilichojeruhiwa liko katika jumba la makumbusho huko Kairo. Kijana wake farao Ahmose (aliyetawala 1580-1558 K.K.) pamoja na ndugu yake Kamose walifaulu na kuwafukuza wa Hyksos toka Misri.


Farao Amenhotepi I (alitawala 1558-1525 K.K.) aliyemfuatia farao Ahmose, alianza kuwatesa sana wana wa Israeli. Aliogopa kwamba Waisraeli watakapopata nguvu zaidi watawatawala Wamisri na kuwaweka chini ya utawala wao, kama watu wa Hyksos walivyofanya kabla.

 

1558-1447 K.K.

KUTOKA. Ilichukua miaka 111.

 

1558 K.K.

Farao Amenhotepi I (1558-1525) alichukua utawala. (KUT 1:8)

 

1531 K.K.

Haruni alizaliwa.

 

1529 K.K.

Farao Amenhotepi I alitoa amri: "Watoto wa Waisraeli wote wakiume watupwe mtoni, mto Nile." (KUT 1:22)

 

1528 K.K.

Musa alizaliwa. Binti wa farao Amenhotepi I (jina lake Hatsepsuti) alimchukua mtoto Musa. (KUT 2)

 

1525 K.K.

Farao Amenhotepi I alifariki na farao Thotmesi I (1525-1508) alichukua utawala. Musa alikuwa na miaka 3.

 

1508 K.K.

Farao Thotmesi I alifariki na farao Thotmesi II (1508-1504) alichukua utawala. Musa alikuwa na miaka 20.

 

1504 K.K.

Farao Thotmesi II alifariki. Musa alikataa kuwa farao. (EBR 11:24) Hatsepsuti, mama yake wa kambo alichukua utawala (1504-1492).

Wakati huo alizaliwa Thotmesi III, mtoto wa dada au wa kaka yake Hatsepsuti.

 

1497 K.K.

Yoshua alizaliwa.

 

1487 K.K.

Musa alianza kuwatetea Waebrania waliokuwa watumwa Misri. Musa alikuwa kinyume cha Wamisri.

Farao Hatsepsuti akaogopa kwamba Musa, atakapokuwa mfalme, angehamisha utawala kutoka Misri kwenda kwa Waebrania yaani wa Waisraeli.

Ili mambo hayo yasifanyike, Hapsepsuti alitoa amri Musa auawe.

Musa akakimbia mpaka Midiani. (KUT 2:11-15)

 

1482 K.K.

Farao Thotmesi III (1482-1450) alichukua utawala.

 

1450 K.K.

Farao Amenhotepi II (1450-1425) alichukua utawala.

 

1448 K.K.

Musa mbele ya kijiti cha moto. (KUT 3)

Musa alirudi Misri.

Mapigo.

Waisraeli walitoka Misri. (KUT 3-12)

 

1448-1408 K.K.

Safari ya wana wa Israeli kutoka Misri jangwani kwenda nchi ya ahadi.

 

1447 K.K.

Kujengwa kwa Hema ya kukutania. (KUT 25-40)

Mwisho wa KUTOKA.

MAMBO YA WALAWI.

 

1446-1408 K.K.

HESABU. Ilichukua miaka 38.

Misri Farao Thotmesi IV alitawala (1425-1405) na baadaye farao Amenhotepi III alitawala (1405-1370). Mke wake malkia Teje.

 

1408 K.K.

KUMBUKUMBU LA TORATI

Kifo cha Haruni na Musa. (HES 20:28, KUM 34:5)

 

1408-1387 K.K.

KITABU CHA YOSHUA. Ilichukua miaka 21.

 

1408 K.K.

Chini ya uongozi wa Yoshua wana wa Israeli waliingia nchini Israeli. Kutekwa kwa Yeriko. (YOS 6)

 

1402 K.K.

Nchi iligawanywa kati ya makabila ya Israeli. (YOS 13-21)

 

1401 K.K.

Hema ya kukutania ilisimimishwa Shilo. (YOS 18:1)

 

1400 K.K.

Makabila ya Reubeni, Gadi na upande wa pili wa kabila la Manase walirudi mashariki ya Yordani. (YOS 22)

 

1387 K.K.

Yoshua alifariki akiwa na miaka 110. (YOS 24:29)

Kumalizika kwa kitabu cha YOSHUA.

 

1387-1070 K.K.

KITABU CHA WAAMUZI. Ilichukua miaka 317.

 

Waisraeli walianza kumsahau Mungu polepole. (AMU 3:12-14)

Farao Amenhotepi IV, yaani Ekhnaton, alitawala nchi ya Misri (1370-1352). Mama malkia Teje. Mke Nefertiti.

 

1368 K.K.

Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia aliwatesa wana wa Israeli. (AMU 3:8)

 

1360 K.K.

Kijana wa ndugu yake Kalebu, Othnieli aliwapa uhuru Waisraeli. (AMU 3:10) Othnieli akiwa mwamuzi. Amani miaka 40.

 

Waamuzi walitawala sehemu mbali mbali za Israeli, na wachache kwa wakati moja.

Ndiyo maana miaka inalaliana na hata hivyo hatuna uhakika na miaka kamili. (AMU 3:10)

 

1320 K.K.

Egloni mfalme wa Moabu aliwatesa wana wa Israeli.

Na aliteka mji wa Mitende, yaani Yeriko. (AMU 3:12-14)

 

1302 K.K.

Ehudi Mbenyamini mwenye mkono wa kushoto, aliwapa uhuru Waisraeli, na alimwua mfalme Egloni. (AMU 3:15-30) Ehudi akiwa mwamuzi na baada yake Shamgari. Wakati wa amani ulichukua miaka 80. (AMU 3:31)

 

1222 K.K.

Mfalme aliyetawala kaskazini mwa Palestina mfalme wa Kanaani Yabini pamoja na mkuu wa jeshi Sisera, waliwatesa wana wa Israeli. (AMU 4:1-3)

 

1202 K.K.

Baraka aliondoka kwenda kupigana na Sisera baada ya kuambiwa na hakimu wa kike nabii Debora. Israeli ilipata uhuru. (AMU 4:4-24) Wimbo wa Debora. (AMU 5) Amani ilikuwepo miaka 40. (AMU 5:31)

 

1162 K.K.

Wamidiani waliwatesa Waisraeli. (AMU 6:1-6)

Gideoni, yaani Yerubaali, aliwashinda Wamidiani akiwa na wanajeshi 300. (AMU 6:11-7:25)

 

Abimeleki, mwana wa Gideoni, alikuwa mfalme. (AMU 9)

Tola alikuwa mwamuzi miaka 23. (AMU 10:1,2)

Yairi alikuwa mwamuzi miaka 22. (AMU 10:3-5)

Wana wa Israeli walimkosea tena Mungu. Waliabudu Baali na Ashtorehti na miungu mingine. Mungu akawatia mikononi mwa Wafilisti na Waamori kwa miaka 18. Waisraeli walimlilia Mungu. (AMU 10:6-18)

 

1115-1012 K.K.

KITABU CHA KWANZA CHA SAMWELI. Kilichukua miaka 103.

1115 K.K.

Samweli alizaliwa. (1SAM 1)

 

1112 K.K.

Yeftha aliwashinda maadui wa Israeli. Akawa mwamuzi Israeli kwa miaka 6. (AMU 11:1-12:7)

 

Ibzani wa Bethlehemu alikuwa mwamuzi kwa miaka 7. (AMU 12:8-10)

Eloni alikuwa mwamuzi kwa miaka 10. (AMU 12:11-12)

Abdoni Mpirathoni alikuwa mwamuzi kwa miaka 8. (AMU 12:13-15)

 

1077 K.K.

Wafilisti waliwashinda Waisraeli na kuiba Sanduko la Agano. (1SAM 4)

Kuhani Eli alifariki. (1SAM 4)

 

Samsoni na Delila. (AMU 16:4-31) Samsoni mwamuzi kwa miaka 20. (AMU 13-16)

 

Sura za mwisho za KITABU CHA WAAMUZI (AMU 17-21) mambo yake yalitokea kabla ya sura za mwanzo.

 

1070 K.K.

Mwisho wa KITABU CHA WAAMUZI. Ilichukua miaka 317.

KITABU CHA RUTHU kilianza wakati wa KITABU CHA WAAMUZI. (RUT 1:1)

 

1056 K.K.

Waisraeli waliwashinda Wafilisti waliokuwa wamewatesa kwa miaka 20. (1SAM 7)

 

1052 K.K.

Sauli alifanywa kuwa mfalme. (1SAM 10)

 

1042 K.K.

Daudi alizaliwa.

(Dada na ndugu za Daudi 1NYA 2:13-16 na 2SAM 17:25)

 

1026 K.K.

Daudi alipakwa mafuta kuwa mfalme. (1SAM 16)

 

1024 K.K.

Daudi na Goliathi. (1SAM 17)

Sauli alianza kumchukia Daudi. Daudi anaoa binti wa Sauli Mikali. (1SAM 18:15-27)

 

1017 K.K.

Samweli alikufa.(1SAM 25:1)

 

1012 K.K.

Wana wa Sauli Yonathani, Abinadabu na Malkishua waliuawa na Wafilisti. (1SAM 31:2)

Sauli alijaribu kujiua. (1Sm 31:4, 1NYA 10)

KITABU CHA KWANZA CHA SAMWELI kilimalizika.

 

1012-972 K.K.

KITABU CHA PILI CHA SAMWELI. Kilichukua miaka 40.

KITABU CHA KWANZA CHA MAMBO YA NYAKATI Kilichukua miaka 40. (Miaka inahesabiwa tangu sura ya 10)

Mwamaleki kijana alimwua Sauli, aliyeumia wakati alipojaribu kujiua. (2SAM 1:5-10)

Daudi alifanywa mfalme wa Yuda. (2SAM 2:4)

Ishboshethi mwana wa Sauli akawa mfalme juu ya sehemu ingine ya Israeli. (2SAM 2:8-10)

 

1010 K.K.

Ishboshethi aliuawa. Daudi aliwaadhibu wauaji. (SAM 4)

 

1005 K.K.

Daudi aliwekwa kuwa mfalme juu ya Israeli yote. Yerusalemu ikawa mji mkuu. (2SAM 5:3, 1NYA 11:1-3)

 

980 K.K.

Absalomu mwana wa Daudi alijaribu kuchukua utawala kwa njia ya vurugu.(2SAM 15-18)

 

973 K.K.

Rehoboamu, mwana wa Sulemani alizaliwa. (2NYA 12:13)

 

972 K.K.

Sulemani alikuwa mfalme. (1FAL 1, 1NYA 29:28)

Daudi alikufa. (1FAL 2:10, 1NYA 29:26-28)

KITABU CHA PILI CHA SAMWELI kilimalizika.

KITABU CHA KWANZA CHA MAMBO YA NYAKATI kilimalizika.

Mungu alitokea Sulemani. (1FAL 3:5-14)

 

972-853 K.K.

KITABU CHA KWANZA CHA WAFALME. Kilichukua miaka 119.

 

972-538 K.K.

KITABU CHA PILI CHA MAMBO YA NYAKATI.

Kilichukua miaka 434.

 

968 K.K.

Sulemani alianza kujenga Hekalu katika mwaka wa 480 baada ya Israeli kutoka Misri. (968+480=1448 = mwaka wa Israeli kuondoka Misri) (1FAL 6, 2NYA 2)

 

961 K.K.

Hekalu lilikamilika. (1FAL 6:38) Ufunguzi. (1FAL 8, 2NYA 6)

 

960 K.K.

Sulemani alianza kujenga nyumba yake. (1FAL 7:1)

 

947 K.K.

Nyumba ya Sulemani ilikamilika. (1FAL 7, 2NYA 8:1)

Bwana alimtokea Sulemani tena mara ya pili.(1FAL 9:1-9, 2NYA 7:11-22)

 

Malkia wa Sheba alienda kumsalimia Sulemani. (1FAL 10, 2NYA 9)

Sulemani alimwacha Mungu. (1FAL 11:1-11)

KITABU CHA MHUBIRI. Kinaeleza juu ya mawazo ya Sulemani ya kipotofu.

 

932 K.K.

Sulemani alifariki. (1FAL 11:43, 2NYA 9:30-31)

 

Utawala uligawanyika:

Israeli ya Kaskazini, na Israeli ya Kusini, yaani Yuda.

(1FAL 12, 2NYA 10)

 

Ni vigumu kujua miaka kamili ya utawala wa wafalme wa Israeli ya kaskazini na Yuda pia, kwani mara nyingi mtoto alianza utawala hata kabla ya kifo cha baba. Hivyo hatuna uhakika na miaka.

 

931-722 K.K.

Wafalme wa Israeli ya Kaskazini:

 

Yeroboamu I, (931-910 K.K.) alikuwa mfalme Israeli ya kaskazini miaka 22. Alifanya mabaya. (1FAL 12:20-14:21) Manabii wakati wa Yeroboamu: Mtu wa Mungu (Yeddo?) (1FAL 13:1-32). Ahia. (1FAL 14:2-18).

 

Nadabu, (910-909 K.K.) mwana wa Yeroboamu, alikuwa mfalme miaka 2. Alifanya mabaya. (1FAL 14:20, 15:25-28)

 

Baasha, (909-886 K.K.) Mwisakari, alimwua Nadabu, akawa mfalme miaka 24. Alifanya mabaya. (1FAL 15:27-16:6) Nabii alikuwa Yehu.

 

Ela, (886-885 K.K.) mwana wa Baasha, alitawala miaka 2. Alifanya mabaya. (1FAL 16:6-10,13,14) Nabii alikuwa Yehu.

 

Zimri, (885 K.K.) alikuwa mfalme siku saba. Alimwua Ela. Aliua jamaa yote ya Baasha. Alifanya mabaya. Alijiunguza na moto hadi akafa. (1FAL 16:9-20)

 

Omri, (885-874 K.K.) alitawala miaka 12. Alianzisha Samaria. Alifanya mabaya zaidi ya wale waliotangulia. (1FAL 16:16-28)

 

Ahabu, (874-853 K.K.) mwana wa Omri, miaka 22. Mke wake Yezebeli. Ahabu aliabudu Baali. Alifanya mabaya. (1FAL 16:28-22:40) Wakati wake, nabii Eliya alitabiri.

 

Ahazia, (853-852 K.K.) mwana wa Ahabu, miaka 2. Alifanya mabaya. (1FAL 22:51-53)

 

Yoramu, (852-841 K.K.) mwana wa Ahabu, miaka 12. Alifanya mabaya. Manabii Mikaya mwana wa Imla na Elisha walikuwa manabii wakati wa Yoramu. (2FAL 3:1-, 6:26-7:20, 8:28-, 29, 9:15-24)

 

Yehu, (841-814 K.K.) alitawala miaka 28. Aliteketeza jamaa ya Ahabu. Akafutilia mbali kuabudu Baali. Nabii alikuwa Elisha. (2FAL 9-10)

 

Yehoahazi, (814-798 K.K.) mwana wa Yehu, miaka 17. Alifanya mabaya. (2FAL 13:1-9)

Yehoashi, (Yoashi) (798-782 K.K.) mwana wa Yehoahazi, miaka 16. Alipigana na mfalme wa Yuda Amazia na alimshinda. Alifanya mabaya. (2FAL 13:9-25, 14:8-16)

 

Yeroboamu II, (782-753 K.K.) mwana wa Yehoashi , alitawala miaka 41. Alifanya mabaya. (2FAL 14:16, 23-29) Manabii walikuwa Yona, Amosi na Hosea.

 

Zekaria, (753-752 K.K.) mwana wa Yeroboamu alitawala nusu mwaka. Alifanya mabaya. (2FAL 15:8-11) Nabii alikuwa Hosea.

 

Shalumu, (752 K.K.) mwezi 1. Alimwua Zekaria. (2FAL 15:10-15) Nabii alikuwa Hosea.

 

Menahemu, (752-742 K.K.) miaka 10. Alimwua Shalumu. Alifanya mabaya. (2FAL 15:14-22) Nabii alikuwa Hosea.

 

Pekahia, (742-740 K.K.) mwana wa Menahemu, miaka 2. Alifanya mabaya. (2FAL 15:23-26) Nabii alikuwa Hosea.

 

Peka, (740-732 K.K.) alitawala miaka 20. Alimwua Pekahia. Alifanya mabaya. (2FAL 15:25-30) Nabii alikuwa Hosea.

 

Hoshea (732-723/722 K.K.) alikuwa mtawala wa mwisho wa Israeli ya kaskazini. Alitawala miaka 9. Alimwua Peka. Alifanya mabaya. Alichukuliwa mateka Ashuru. (2FAL 15:30, 17:1-6) Nabii alikuwa Hosea.

 

722 K.K.

Kumalizika kwa Waisraeli walihamia Ashuru.

 

931-586 K.K.

Wafalme wa Israeli ya Kusini, yaani Yuda:

 

931 K.K.

Rehoboamu, (931-914) mwana wa Sulemani, alikuwa mfalme wa Yuda miaka 17. Alifanya mabaya. (1FAL 12:1-24, 14:21-31, 2NYA 10-12) Nabii alikuwa Shemaya. (1FAL 12:22-24)

 

925 K.K.

Farao Shishaki alitawala Yerusalemu na aliwaibia. (1FAL 14:25,26)

 

Abiya, (913-911) mwana wa Rehoboamu alitawala miaka 3. Alifanya mabaya. (1Kn 15:1-8, 2Ak 13:1-14:1) Nabii alikuwa Iddo.

 

Asa, (911-870) mwana wa Abiya alitawala miaka 41. Alifanya mema. Manabii walikuwa Asaria na Hanani. (1FAL 15:8-24, 2Ak 14-16)

 

Yehoshafati, (870-848) mwana wa Asa, alitawala miaka 25. Mama yake alikuwa Azuba. Alifanya amani na Israeli. Alifanya mema. (1FAL 22:41-51)

 

Yehoramu, (848-841) mwana wa Yehoshafati alitawala miaka 8. Mkewe binti wa Ahabu. Alifanya mabaya. (1FAL 22:51, 2FAL 8:16-24) Nabii alikuwa Obadia.

 

Ahazia, (841) mwana wa Yehoramu mwaka 1. Yehu mfalme wa Israeli alimwua. Ahazia alifanya mabaya. (2FAL 8:25-29, 9:16-29)

 

Athalia, (841-835) mamaye Ahazia alitawala miaka 6. Alikuwa mtawala mbaya sana. (2FAL 11:1-20)

 

Yoashi, (835-796) mwana wa Ahazia alitawala miaka 40. Alifanya mema. (2FAL 12:1-21) Manabii walikuwa Yoeli na Zekaria.

 

Amazia, (796-767) mwana wa Yoashi alitawala miaka 29. Alifanya mema. (2FAL 14:1-20) Nabii alikuwa Zekaria.

 

Azaria, yaani Uzia, (767-740) mwana wa Amazia alitawala miaka 52. Alifanya mema. Aliugua muda mrefu, hakuweza kutawala mwishoni. (2FAL 4:21,22,15:1-7) Nabii alikuwa Isaya.

 

Yothamu, (750/740-735) mwana wa Azaria alitawala miaka 16. Alifanya mema. (2FAL 15:32-38) Manabii walikuwa Isaya na Mika.

 

Ahazi, (732-716) mwana wa Yothamu miaka 16. Hakufanya mazuri. (2FAL 15:38-16:20) Manabii walikuwa Isaya na Mika.

 

722 K.K.

Israeli ya Kaskazini ilihamishwa Ashuru. Israeli ya Kaskazini haikuwepo tena. (2FAL 17)

 

Hezekia, (716-687 K.K.) mwana wa Ahazi alitawala miaka 29. Alifanya mazuri. Aliugua lakini aliongezewa maisha miaka 15. (2FAL 18:1-20:21) Manabii walikuwa Isaya na Mika.

 

Manase, (687-643 K.K.) mwana wa Hezekia alitawala miaka 55. Alifanya mabaya. Baadaya alinyenye kea. (2FAL 21:1-18) Nabii alikuwa Isaya.

 

Amoni, (643-641 B.K.) mwana wa Manase alitawala miaka 2. Alifanya mabaya. (2FAL 21:18-26)

 

Yosia, (641-609 K.K.) mwana wa Amoni alitawala miaka 31. Alifanya mema. Aliimarisha ibada. Ulikuwa wakati wa uamusho Yuda. Farao-neko alimwua. (2FAL 22:1-23:30) Manabii walikuwa Nahumu, Habakuki, Sefania, Yeremia na Hulda walitabiri wakati wa Yosia.

 

Yehoahazi, (609 K.K.) mwana wa Yosia alitawala miezi 3 tu. Alifanya mabaya. Farao-neko alimweka kifungoni na akampeleka Misri. (2FAL 23:30-34) Manabii walikuwa Yeremia na Habakuki.

 

Yehojakimu, (= Eliakimu) (609-598 K.K.) mwana wa Yosia, ndugu wa Yehoahazi alitawala miaka 11. Alifanya mabaya. (2FAL 23:34-24:6) Nabii alikuwa Yeremia.

 

605-562 K.K.

Nebukadreza alitawala Babeli.

 

604 K.K.

Danieli pamoja na wengine wa jamii ya kifalme walihamishiwa katika uhamisho wa lazima Babeli. (DAN 1:1-6)

 

Yekonia, (598/597 K.K.) mwana wa Yehoyakimu alitawala miezi 3 tu. Alifanya mabaya. Nebukadreza aliteka Yerusalemu na kuchukua vitu vya Hekalu na sehemu kubwa ya watu wa Yerusalemu akawapeleka Babeli. (2FAL 24:6-15) Nabii Yeremia.

 

Ezekieli alipelekwa Babeli. Alitabiri miaka 593-570 K.K.

 

Sedekia, (=Matania) (597-586 K.K.) ndugu ya baba yake Yekonia alitawala miaka 11. Alifanya mabaya. (2FAL 24:17-25:7) Nabii Yeremia.

 

588 K.K.

Nebukadreza alianza kuizunguka Yerusalemu. (2FAL 25:1)

 

586 K.K.

Yerusalemu ilitekwa. Mji na Hekalu viliteketezwa. Sedekia na watu na sehemu kubwa walipelekwa Babeli. (2FAL 25:2-4)

 

582 K.K.

Sehemu ya mwisho ya wafungwa walihamishiwa Babeli.

 

560-480 K.K.

Budha (Bara-Hindi)

 

551-478 K.K.

Konfutse (Uchina)

 

539 K.K.

Koreshi alitawala Babeli. Utawala wa Babeli uliharibika. (2NYA 36:21-) Uajemi ikawa utawala wa dunia nzima mpya.

 

538 K.K.

Wayahudi kama 50.000 walirudi Yerusalemu kufuatia wito wa Zerubabeli. (2NYA 36:22,23)

 

537 K.K.

Msingi wa Hekalu ulijengwa. Kazi ilisimamishwa.

 

536 K.K.

Maono ya mwisho wa kitabu cha Danieli.

 

520 K.K.

Ujenzi wa Hekalu ulianza tena. Manabii walikuwa Hagai na Zekaria.

 

516 K.K.

Zerubabeli alifungua Hekalu.

 

486-465 K.K.

Ahasuero (Kserkses I) alikuwa mtawala wa Uajemi.

Kitabu cha ESTA. (Kilichukua miaka 21)

 

485-425 K.K.

Myunani Herodotos mwandishi wa historia.

 

480 K.K.

Esta akawa malkia.

 

470-399 K.K.

Myunani Sokrates mfilosofia.

 

457 K.K.

Ezra aliingia Yerusalemu pamoja na Wayahudi 2000.

 

445 K.K.

Nehemia alienda kutengeneza kuta za Yerusalemu. Nabii alikuwa Malakia.

 

428-348 K.K. Platon.

 

384-322 K.K. Aristoteles.

 

 

Vitabu vya Agano la Kale:

 

Miaka kabla ya Kristo (K.K.)

 

MWANZO. Tangu mwanzo hadi mwaka wa 1807 K.K.

KUTOKA 1558-1447 K.K. (Kilichukua miaka 111)

MAMBO YA WALAWI 1446. K.K.

HESABU 1446-1408 K.K. (Kilichukua miaka 38)

KUMBUKUMBU LA TORATI 1408.K.K.

YOSHUA 1408-1387. K.K. (Kilichukua miaka 21)

WAAMUZI 1387-1070. K.K. (Kilichukua miaka 317)

RUTHU yanatokea wakati wa Waamuzi. (RUT 1:1)

1. SAMWELI. 1115-1012 K.K. (Kilichukua miaka 103)

2. SAMWELI. 1012-972 K.K. (Kilichukua miaka 40)

1. WAFALME. 972-853 K.K. (Kilichukua miaka 119)

2. WAFALME. 853-562 K.K. (Kilichukua miaka 291)

1. MAMBO YA NYAKATI. (Tangu 1NYA 10) 1012-972 K.K. (Kilichukua miaka 40)

2. MAMBO YA NYAKATI. 972-538 K.K. (Kilichukua miaka 434)

EZRA. 538-457 K.K. (Kilichukua miaka 81)

NEHEMIA. 445-432 K.K. (Kilichukua miaka 13)

ESTA. 486-465 K.K. (Kilichukua miaka 21)

AYUBU. Wakati wa Ibrahimu (2168-1993 K.K.)

ZABURI. 1450-500 K.K.

MITHALI. Wakati wa utawala wa Sulemani 972-932 K.K. Na pia baada ya Sulemani.

MHUBIRI. Wakati wa mwisho wa maisha ya Sulemani 935 K.K.

WIMBO ULIO BORA. Wakati wa mwanzo wa utawala wa Sulemani 970 K.K.

ISAYA 739-701. K.K. (au labda hadi mwaka 680 K.K.)

YEREMIA. 627-586 K.K.

MAOMBOLEZO. 586 K.K.

EZEKIELI alizaliwa 623 K.K. Alipelekwa Babeli 598, alitabiri 593-570 K.K.

DANIELI alizaliwa 622 K.K. Alipelekwa Babeli 604, alitabiri Babeli mpaka mwaka wa 536. K.K.

HOSEA aliishi miaka ya 770-700 K.K. Alikuwa nabii miaka ya 750-722 K.K.

YOELI aliishi Yuda katikati miaka ya 800 na 700 K.K.

AMOSI alitabiri Kusini mwa Israeli 765-750 K.K.

OBADIA muda wa kazi haujulikani. Labda mwaka wa 850 au 586 K.K.

YONA aliishi katikati miaka ya 800 na 700 K.K.

MIKA alitabiri 730-680 K.K.

NAHUMU, HABAKUKI na SEFANIA walitabiri wakati wa Yosia 640-609 K.K.

HAGAI na ZEKARIA miaka 520 K.K.

MALAKI kama miaka 425 K.K. Nabii wa mwisho wa Agano la Kale.

 

Miaka 400 ilipita kati ya Agano la Kale na Agano Jipya.

Persia ilitawala baada ya Babyloni na 330 K.K. Ugiriki iliimarika.

Mwaka wa 100 Wayahudi walijaribiwa kuwageuza wawe Wagiriki kwa lazima.

Wayahudi walipambana na Wagiriki lakini Wayahudi hawakufanikiwa.

Septuaginta (jina la Agano la Kale tafsiri ya Kigirigi) ilikamilika mwaka wa 150 K.K.

Polepole Warumi walipata nguvu na mwaka wa 63 K.K. Waisraeli walichukuliwa chini ya utawala wa Rumi.

 

Miaka ya utawala duniani:

 

Babeli 604-539 K.K.

Uajemi 539-332 K.K.

Ugiriki, yaani Uyunani 332-320 K.K.

Misri 320-198 K.K.

Siria 198-165 K.K.

Wamakabi na Wahasmoni 165-63 K.K. (Israeli)

Warumi waliteka Israeli 63 K.K.

 

37-4 K.K. Herode mkuu mfalme wa Palestina.

 

19 K.K. Ujenzi wa Hekalu la Yerusalemu ulianzishwa.

 

 

Agano la Kale lilimalizika.


Wakati wa Agano Jipya ulianza.

 

Matukio ya Agano Jipya:

 

5 K.K. Yesu alizaliwa.

8 B.K. (= baada ya Kristo) Yesu aliingia katika Hekalu Yerusalemu akiwa na miaka 12.

26 B.K. Yohana mbatizaji alianza kuhubiri.

26-30 B.K. Kazi ya Yesu.

31 B.K. Kifo cha Anania na Safira.

33 B.K. Kifo cha Stefano.

33/34 B.K. Sauli yaani Paulo alibadilika.

34-42 B.K. Paulo Uarabuni, Dameski, Yerusalemu na Tarso.

42 B.K. Paulo aliwekwa kuwa mchungaji wa kanisa la Antiokia.

44 B.K. Mtume Yakobo alikufa kifo cha mfia dini, Petro alitoka gerezani ki-miujiiza.

45-48 B.K. Safari ya kwanza ya Paulo ya kimisheni.

50-53 B.K. Safari ya pili ya Paulo ya kimisheni.

54-58 B.K. Safari ya tatu ya Paulo ya kimisheni.

58-60 B.K. Paulo aliwekwa kifungoni Kaisaria.

61-63 B.K. Paulo alifungwa Rumi.

67 B.K. Paulo na Petro waliuawa.

98 B.K. Mtume Yohana alifariki.

100 B.K. Wakati wa Mitume ulikwisha.

590-1517 B.K. Ukatoliki uliendelea.

570-632 B.K. Muhamedi

1517- B.K. Kanisa la kiprotestanti lilianza.

1900 B.K. Uamsho wa Pentekoste ulianza.

 

Vitabu vya Agano Jipya:

 

Mwaka wa vimeandikwa:

 

MATHAYO 50 B.K.

MARKO 64-68 B.K.

LUKA 58 B.K.

YOHANA 90 ? B.K.

MATENDO 63 B.K.

WARUMI 57/58 B.K.

1. WAKORINTHO 54/55 B.K.

2. WAKORINTHO 57 B.K.

WAGALATIA 53 B.K.

WAEFESO 61/62 B.K.

WAFILIPI 62 B.K.

WAKOLOSAI 62 B.K.

1. WATHESALONIKE 50 B.K.

2. WATHESALONIKE 52 B.K.

1. TIMOTHEO 63-67 B.K.

2. TIMOTHEO 67 B.K.

TITO 63-67 B.K.

FILEMONI 62 B.K.

WAEBRANIA kabla ya 70 B.K.

YAKOBO 45-50 B.K.

1. PETRO 65 B.K.

2. PETRO 67 B.K.

1. YOHANA 85-90 B.K.

2. YOHANA 85-90 B.K.

3. YOHANA 85-90 B.K.

YUDA 66/67 B.K.

UFUNUO 95 B.K.

 



Copyright Teuvo Kopra

 Emaili yangu





WebDesign Miia Metsola